
Charles Aranguiz alianza kuipatia Chile bao la mapema ikiwa ni dakika ya tatu tangu mchezo huo kuanza kabla ya winga wa Arsenal Alexis Sanchez kufunga goli la pili dakika ya 37 na kuifanya Chile iende mapumziko ikiwa mbele kwa goli 2-0 dhidi ya Bolivia.

Aranguiz alipachika pao la tatu kwa Chile dakika ya 66 lakini likiwa ni bao lake la pili kwenye mchezo huo, kabla Gary Medel hajatupia nyavuni goli la nne dakika ya 80. Zikiwa zimebaki dakika nne ili mwamuzi amalize pambano hilo, Raldes wa Bolivia alijifunga na kuufanya mchezao huo kumalizika kwa wenyeji wa mashindano (Chile) kuibuka na ushindi mnono wa goli 5-0.
Aturo Vidal alikuwepo kwenye kikosi kilichoifanyia mauaji Bolivia akitokea kwenye sekeseke la ajali ambayo aliipata kutokana na kuendesha gari kwa spidi kali huku akiwa amelewa. Lakini tofauti na matarajio ya wengi, Vidal bado alipata sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki wa Chile ambao wamefurahia pia timu yao kusonga mbele kwa hatua ya robo fainali kwenye michuanon hiyo.

Miller Bolanos alianza kuipatia Ecuador bao la kuongoza dakika ya 26 kabla ya mshambuliaji wa West Ham Enner Valencia kuongeza goli la pili dakika ya 57 kwa upande wa Ecuador. Mexico walipata goli lao la kufutia machozi dakika ya 64 kwa mkwaju wa penati uliowekwa kambani na Raul Jimenez.